WAWILI WASHTAKIWA KWA MAUAJI ELDORET

Watu wawili wanaodaiwa kumuua mwanamume wa makamo miezi kadhaa iliyopita kwa kushukiwa kuwa jambazi wameshtakiwa kwa mauaji katika mahakama kuu ya Eldoret.
Robert Kiplagat, mkulima mdogo na Alex Kiptoo, mwanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Udaktari cha Kenya (KMTC) katika chuo kikuu cha Nairobi walipofika mbele ya Jaji Robert Wananda wakukanusha shtaka moja la mauaji.
Mahakama iliyojaa watu ilisikia kwamba walitenda kosa hilo mnamo Aprili 6, 2024, eneo la HZ Keiyo Kusini, Kaunti ya Elgeyo Marakwet.
Imetayarishwa na Janice Marete