WASALITI NAMBA MOJA; LSK WAAMBIA WABUNGE
Chama cha wanasheria nchini LSK kimewasuta wabunge wa bunge la kitaifa kwa madai kwamba wamewafeli wakenya.
Kwa mujibu wa rais wa LSK Faith Odhiambo wabunge wamekuwa wakitumika kutimiza ajenda za serikali badala ya kutimiza agenda za mwananchi mpiga kura.
Odhiambo vile vile ametumia fursa hiyo kuwasuta viongozi na serikali kwa jumla kwa kupelekea wakosa kukosa imani nao hatua ambayo imepelekea wao kuandamana.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































