GACHAGUA: RUTO HAFAMU CHANGAMOTO ZA NCHI
Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua amemkosoa Rais William Ruto kwa kuzilaumu taasisi mbali mbali na kuzihusisha na maandamano yanayoongozwa na vijana wa kizazi cha Gen Z.
Akizungumza katika jimbo la Massachusetts nchini Marekani, Gachagua amesisitiza haja ya Rais William Ruto kuondolewa mamlakani ifikapo mwaka wa 2027.
Gachagua amedai kuwa Rais Ruto hana ufahamu kuhusu changamoto zinazoikabili nchi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































