KAYOLE STARLETS KUWAKILISHA KENYA
Kocha mkuu wa Kayole Starlets Mary Adhiambo ameeleza fahari yake baada ya wachezaji wake watatu kuchaguliwa kuwakilisha Kenya kwenye Kombe la Dunia la Wasio na Makazi 2025, lililoratibiwa kuandaliwa Oslo, Norway, kuanzia Agosti 23 hadi 30, 2025.
Kikosi cha Ligi Kuu ya Wanawake kitakuwa na Lavyne Achola, Rose Mumbua, na Mercy Mung’uro kupamba rangi za kitaifa katika shindano la kipekee la kimataifa ambalo huleta pamoja wachezaji ambao hawana makao au ambao hapo awali walikumbwa na ukosefu wa makazi.
Kocha Adhiambo alipongeza kuitwa kwa wachezaji hao kama fursa kubwa kwa watatu hao, akisema kutawaweka wazi katika soka la kimataifa na pia kuwasaidia kushindana na timu zilizo na uzoefu zaidi.he Homeless World Cup ni mashindano ya kila mwaka ambayo yanalenga kuongeza uelewa kuhusu ukosefu wa makazi na kutetea umuhimu wa kusaidia jamii zilizo hatarini.
Timu zote za wanaume na wanawake hushiriki, mechi zikichezwa chini ya muundo maalum: wachezaji wanne kwa kila upande na muda wa dakika 14 pekee kwa kila mchezo.
Mwaka huu, timu ya wanawake ya Kenya imepangwa Kundi C pamoja na mabingwa watetezi Mexico, Ireland Kaskazini, Sweden, Ugiriki na Zimbabwe.
Mashindano hayo yaliandaliwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2003 huko Graz, Austria yaliyoandaliwa na Wakfu wa Kombe la Dunia la Wasiokuwa na Makazi yenye makao yake makuu huko Scotland. Kila mwaka, nchi tofauti huandaa hafla hiyo.
imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































