#uncategorized

KENYA KUKABANA KOO NA MADAGASCAR

Mbio za Kenya katika michuano yao ya kwanza ya Mataifa ya Afrika (CHAN) zinakabiliwa na jaribu kali zaidi bado watakapomenyana na Madagascar katika robo fainali katika Uwanja wa Kimataifa wa Michezo wa Moi, Kasarani, Ijumaa, Agosti 22.

Harambee Stars chini ya kocha Benni McCarthy inaoongoza Kundi ‘A’ bila kushindwa baada ya kulaza Zambia 1-0 katika mechi yao ya mwisho ya kundi.

Lakini historia inaonyesha kwamba Barea ya Madagaska si wageni kwa kikosi cha harambee stars.

Pande hizo mbili zimekutana mara moja kwa mechi ya kirafiki ya kimataifa mnamo Juni 7, 2019 – ambapo Kenya ilishinda 1-0 kupitia kwa mkwaju wa penalti wa dakika ya 64 Victor Wanyama.

Madagaska iliyoko nafasi ya 115 ya FIFA, nafasi sita tu chini ya Kenya (109), itawasili ikiwa na ari na uthabiti wa kushinda .

Safari ya madagaska ya hatua ya makundi haikuwa ya moja kwa moja: sare ya 1-1 dhidi ya Mauritania licha ya kucheza mtu chini, ikifuatiwa na kufungwa 2-1 na wenyeji wenza Tanzania. Huku kampeni yao ikielekea ukingoni, waliibuka tena, na kuishinda Jamhuri ya Afrika ya Kati 2-0 kabla ya kufuzu kwa ushindi mnono wa 2-1 dhidi ya Burkina Faso.

Matokeo hayo yamejihakikishia nafasi ya pili katika Kundi ‘B’, nyuma ya Tanzania ambayo haijafungwa

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KENYA KUKABANA KOO NA MADAGASCAR

MALKIA STRIKERS WATIA KASI KWA MAZOEZI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *