BARASA AMKOSOA UHURU
Gavana wa Kakamega Fernandes Barasa amekosoa madai ya Rais mstaafu Uhuru Kenyatta kwamba serikali ya Kenya Kwanza inaporomosha mafanikio ya utawala wake.
Akizungumza katika eneo la Navakholo Kaunti ya Kakamega, Barasa amesema kwamba Kaunti ya Kakamega haikupata miradi mikubwa yoyote chini ya uongozi wa Kenyatta na kumtaka Rais Mstaafu kuwacha uongozi wa Serikali ya Kenya kwanza utumikie wakenya.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































