SHULE 29 ZAPOKEA VIFAA VYA MAHABARA BUNGOMA

Zaidi ya shule 29 katika eneo bunge la Webuye magharibi
kaunti ya Bungoma zimepata msaada wa vifaa vya mahabara kutoka shirika la kutengeneza
vifaa vya shule nasepu.
Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo mkurugenzi wa elimu
katika eneo hilo amesema vifaa hivyo vitasaidia pakubwa kufanikisha
utekelezxwaji wa mtaala wa CBC hasa katika
masomo ya sayansi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha walimu wakuu wa
shule za msingi KEBSHA tawi la Bungoma Joseph Sangura amewataka walimu
waliopokea vifaa hivyo kuvitunza na kuvitumia vyema
Imetayarishwa na: Janice Marete