ARSENALI WAWAPIKU REAL MADRID
Ligi ya Premia nchini England itahakikishiwa angalau timu tano katika makala yajayo ya Ligi ya Mabingwa ulaya 2025-26 kufuatia ushindi wa Arsenal wa 3-0 dhidi ya Real Madrid katika mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Jumanne.
EPL ilihitaji ushindi mmoja pekee kutoka kwa vilabu vyake katika mashindano yoyote kati ya matatu ya Ulaya ili kupata moja ya nafasi mbili za ziada – juu ya nne zilizotolewa kwa nchi zilizoorodheshwa zaidi katika safu ya mgawo ya UEFA.
Katika mfumo huu, timu hupata pointi mbili kwa kushinda na moja kwa sare, zikijumlisha pointi zote zilizopatikana kwa kila klabu na kugawanywa kwa idadi ya klabu kutoka ligi hiyo inayoshiriki Ulaya.
England inaweza kuwa na hadi timu saba katika Ligi ya Mabingwa msimu ujao ikiwa Aston Villa itashinda kombe hilo msimu huu bila kufuzu kupitia jedwali la Ligi Kuu, na ikiwa Manchester United au Tottenham Hotspur watatawazwa mabingwa katika Ligi ya Europa.
Italia inaongoza mbio za kuwania nafasi ya pili ya ziada, huku Uhispania na Ujerumani zikiburuza mkia.
Vinara wa Ligi ya Premia, Liverpool na Arsenal wanaoshika nafasi ya pili wanatarajiwa kuambulia nafasi mbili kati ya tano zinazopatikana, huku Nottingham Forest wakishikilia nafasi ya tatu.
Chelsea, Newcastle United, Manchester City, Aston Villa, Brighton & Hove Albion, na Bournemouth iliyo nafasi ya 10 zimetofautishwa na pointi nane.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































