WAPE MTIHANI KAMA WAKO SAWA, OGAMBA
Huku masomo ya vyuo vikuu yakiendelea kuathirika kutokana na mgomo wa wahadhiri, waziri wa elimu Julius Ogamba amewataka wasimamizi wa vyuo hivyo kuwapa wanafunzi mitihani ya mwisho wa muhula iwapo wana uhakika kwamba wanafunzi wamepokea mafunzo ya kutosha.
Akizungumza mapema leo baada ya uzinduzi wa usambazaji wa karatasi za mtihani wa KCSE katika kaunti ya Nyamira, Ogamba amesema wizara yake inasaka suluhu ya kudumu kwa migomo ya mara kwa mara.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































