POLISI WACHUNGUZA MAUAJI HUKO MALAVA
Polisi wameanzisha uchunguzi wa mauaji ya mzee wa miaka 73 katika kijiji cha Ikoli, Malava, huku Mkewe akijeruhiwa vibaya na kulazwa hospitalini.
Inadaiwa washambuliaji walivamia boma lao usiku wa manane, wakimuua mzee huyo na kumkata ulimi mkewe huku ripoti za awali zinaonyesha kuwa marehemu alikataa kutoa hati ya ardhi kwa ndugu zake.
Chifu Moses Namutali amewataka wakazi kuwa watulivu huku uchunguzi ukiendelea. Marehemu ameacha wake wanne na watoto 34.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































