ANDUGU ANA MATUMAINI YA MSIMU UJAO
Katibu Mkuu wa AFC Leopards Gilbert Andugu anatumai kuwa timu hiyo itashinda mechi zao zote zilizosalia ili kumaliza msimu wa ligi kuu ya msimu wa mwaka wa 2023/24 kwa kasi.
Ingwe kwa sasa wako nafasi ya sita kwenye jedwali wakiwa na alama 47, moja nyuma ya Bandari iliyo nafasi ya nne kuelekea Shabana tarehe 15 mwezi huu.
Andugu pia amewahamasisha mashabiki wa Ingwe kujitokeza kwa wingi dhidi ya Shabana ili kuishangilia timu yao wakati ligi hiyo ikikaribia kumalizika.
Imetayarishwa na Nelson Andati.
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































