GAVANA MWANGAZA AZIMIWA, TENA

Gavana wa Meru Kawira Mwangaza ametimuliwa afisini, kwa mara ya tatu katika muda wa miaka 2 baada ya wawakilishi wadi kupiga kura ya kumtimua kutokana na tuhuma za ukiukaji wa katiba, utovu wa nidhamu na matumizi mabaya ya afisi.
Hoja ya kumbandua mamlakani aliwasilishwa katika bunge hilo na naibu kiongozi wa walio wengi Zipporah Kinya, na kuungwa mkono na wawakilishi wadi 49 dhidi ya 17 waliopinga.
Gavana huyo atajua mwisho wake wakati hoja hiyo itawasilishwa katika bunge la seneti kuona iwapo uamuzi huo utabatilishwa au kudumishwa.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa