#Local News

KAULI YA RUTH ODINGA KUHUSU USHIRIKIANO WA ODM-UDA

Bado ni mapema kwa chama cha ODM kuingia kwenye makataba wa kisiasa na UDA kuelekea uchaguzi mkuu ujao, ikizingatiwa kuwa ajenda 10 zilizoafikiwa kati ya Rais William Ruto na kinara mwanzilishi wa ODM marehemu Raila Odinga hazijatekelezwa.

Haya ni kulingana na Ruth Odinga, ambaye ni mwakilishi wa kike wa kaunti ya Kisumu na dadake Odinga, anayetaka ODM kujipanga upya kabla ya kuafikia makubaliano yoyote ya kisiasa.

Kulingana naye, hakuna sababu za makubaliano mapya kabla ya utekelezaji wa ajenda hizo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *