RUTO: UN IFANYIWE MAGEUZI KUZUIA MIGOGORO

Rais William Ruto ameshinikiza mageuzi katika baraza la usalama la umoja wa Mataifa ili kukabili changamoto zinazoibuka.
Kwa mujibu wa Rais Ruto, mfumo uliopo kwa sasa umeshindwa kukabiliana na migogoro inayoibuka hususan suala la mabadiliko ya tabia nchi, kutokuwa na usawa na madeni.
Akizungumza katika mkutano wa marais jijini New York ulioangazia mustakabali wa mataifa wanachama, Ruto amesema mageuzi yatazuia migogoro ya kimataifa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa