#Local News

EACC YAFICHUA ONGEZEKO LA HONGO

Idadi ya wakenya wanaotoa hongo ili kuhudumiwa katika idara za serikali ilipanda hadi asimilia 25 mwaka jana kutoka aslimia 17.7 mwaka wa 2023, idara ya polisi ikiongoza katika kupokea hongo.

Haya ni kwa mujibu wa ripoti ya tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC, asilimia 43 ya waliohojiwa ikikiri kutoa hongo baada ya kuitishwa, asilimia 23 wakiamini kuwa ilikuwa njia ya pekee ya kupata huduma, nayo asilimia 18 ikifanya hivyo ili kurakishiwa huduma.

Idara ya huduma kwa wanyamapori KWS na hazina ya NSSF ni miongoni mwa idara zilizopokea hongo kwa kiwango cha juu.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *