HOFU YA ONGEZEKO LA GHARAMA MBAGATHI
Wabunge wameibua hofu kuhusu kuongezeka kwa gharama ya ujenzi wa hospitali ya rufaa ya huduma ya kitaifa ya polisi ya Mbagathi, ambayo sasa imefikia shilingi milioni 833, kutoka makadirio ya awali ya shilingi milioni 400.
Wakizungumza wakati wa kikao na Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja, wanachama wa kamati ya bunge kuhusu usalama wametaja hatua hiyo kuwa dalili ya ufisadi, mbunge wa Homa Bay Mjini Peter Kaluma, akisema bunge litakomesha mwenendo huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































