#Local News

HOFU YA ONGEZEKO LA GHARAMA MBAGATHI

Wabunge wameibua hofu kuhusu kuongezeka kwa gharama ya ujenzi wa hospitali ya rufaa ya huduma ya kitaifa ya polisi ya Mbagathi, ambayo sasa imefikia shilingi milioni 833, kutoka makadirio ya awali ya shilingi milioni 400.

Wakizungumza wakati wa kikao na Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja, wanachama wa kamati ya bunge kuhusu usalama wametaja hatua hiyo kuwa dalili ya ufisadi, mbunge wa Homa Bay Mjini Peter Kaluma, akisema bunge litakomesha mwenendo huo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *