#Sports

RISING STARLETS WAINGIA AWAMU YA 3, KUMENYANA NA TANZANIA

Timu ya taifa ya soka kwa akina dada wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Starlets wametinga awamu ya 3 kipute cha kufuzu kwa kombe la dunia baada ya kuwachabanga wenzao wa Ethiopia mabao 4-0 katika mkondo wa pili, na hivyo kufikisha jumla ya mabao 5-1.

Katika mechi ya marudiano hapo jana kwenye uwanja wa Ulinzi Sports Complex, Valary Nekesa aliwapa Ulinzi Starlets uongozi kunako dakika ya 4, kabla ya kufunga tena katika dakika ya 69, wafungaji wengine wakiwa Elizabeth Mideva na Fasila Adhiambo

Vipusa hao wa Kenya watamenyana na majirani Tanzania waliotandika Angola jumla ya mabao 7-0, kufuatia ushindi wa mabao 4:0 na mabao 3:0 katika mkondo wa kwanza na wa pili mtawalia.

Imetayarishwa na Nelson Andati

RISING STARLETS WAINGIA AWAMU YA 3, KUMENYANA NA TANZANIA

IEBC YAANZA USAJILI WA WAPIGA KURA

RISING STARLETS WAINGIA AWAMU YA 3, KUMENYANA NA TANZANIA

POLICE FC, NAIROBI UNITED WAFAIDI MABAO YA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *