#Local News

IDADI NDOGO YA WAPIGA KURA YAZUA HOFU

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imeibua hofu kuhusu idadi ndogo ya wapiga kura wapya waliosajiliwa, IEBC ikiripoti kuwasajili wakenya elfu 90 pekee katika kipindi cha mwezi mmoja.

Kwa mujibu wa tume hiyo, kaunti ya Nairobi inaongoza kwa wapiga kura wapya ambao ni 16,000, huku kaunti za Tana River, Marsabit, Isiolo na Samburu zikikosa kufikisha watu 500 katika kipindi hicho.

Viongozi wa kisiasa sasa akiwemo aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua wametoa wito kwa vijana kujisajili.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

IDADI NDOGO YA WAPIGA KURA YAZUA HOFU

POLICE FC WAFYATUA UPYA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *