KIPA WA BURUNDI ASIFIA KIKOSI CHA HARAMBEE STARS

Mlinda lango wa Burundi Jonathan Nahimana amekitaja kikosi cha Harambee Stars kuwa bora zaidi ikilinganishwa na kile cha Burundi.
Kwenye mahojiano na sports boom,Nahimana amekitaja kikosi cha Harambee Stars kuwa na wachezaji bora huku akisema nia yao ni kulipiza kisasi dhidi ya Harambee Stars, ambao waliwashinda katika michuano ya CECAFA Challenge Cup 2017 iliyofanyika nchini Kenya mara ya mwisho walipomenyana.
Nahimana ambaye anachezea timu ya Namungo inayoshiriki ligi kuu ya Tanzania ameichezea Burundi kwa mechi 34, anaamini kwamba nchi zote mbili zina kile kinachohitajika kurejea kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) na kukata tikiti ya kombe la Dunia.
Kipa huyo mwenye uzoefu alikuwa langoni katika mechi ya mwaka wa 2017 na anatarajiwa kuweka nafasi yake katika pambano la kesho Ijumaa 7 dhidi ya Kenya litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa wa Bingu. Kabla ya pambano hilo, Nahimana, ambaye amekuwa mwanzilishi anayependekezwa kwa muda mrefu, anatarajia mechi ngumu na ushindi kwa Burundi mwishoni.
Aidha mlinda lango huyo amesema kuwa matayarisho kwa upande wao yamekuwa bora na wanasubiri kwa hamu na ghamu kutifuana na Kenya.
Imetayarishwa na Nelson Andati