#Local News

KAUNTI ZAONGEZEWA MGAO

Hatimaye vuta nikuvute kuhusu mgao wa serikali za kaunti imepata suluhu baada ya kamati ya Pamoja ya wabunge na maseneta kuafikiana shilingi bilioni 415 kwa serikali hizo kwenye mwaka wa kifedha wa 2025-26.

Mgao huo ni nyongeza ya shilingi bilioni 27.6, kutoka bilioni 387.4 kwenye mwaka huu unaokamilika wa kifedha.

Aidha, hii ni nyongeza ya shilingi bilioni 10 kutoka bilioni 405 zilizokuwa zimependekezwa na wizara ya fedha.

Imetayrishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *