#Local News

GACHAGUA: MAHAKAMA YAMPA PIGO JINGINE

Naibu Rais Rigathi Gachagua sasa atalazimika kufika mbele ya bunge la seneti wakati wa kusikilizwa kwa hoja ya kutimuliwa kwake kutoka afisini baada ya mahakama kuu kudinda kutoa amri ya kusitisha vikao hivyo.

Jaji wa mahakama hiyo Chacha Mwita, ametoa uamuzi huo licha ya Gachagua kupitia kwa mawakili wake kutaka mahakama isitishe vikao hivyo ambavyo vinatarajiwa kuanza hapo kesho.

Kwenye kesi hiyo, mawakili wa Gachagua wanashikilia kwamba hoja ya kutimuliwa kwa mteja wao imechochewa kisiasa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

GACHAGUA: MAHAKAMA YAMPA PIGO JINGINE

ODM IKO IMARA, NYONG’O

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *