GACHAGUA: MAHAKAMA YAMPA PIGO JINGINE
Naibu Rais Rigathi Gachagua sasa atalazimika kufika mbele ya bunge la seneti wakati wa kusikilizwa kwa hoja ya kutimuliwa kwake kutoka afisini baada ya mahakama kuu kudinda kutoa amri ya kusitisha vikao hivyo.
Jaji wa mahakama hiyo Chacha Mwita, ametoa uamuzi huo licha ya Gachagua kupitia kwa mawakili wake kutaka mahakama isitishe vikao hivyo ambavyo vinatarajiwa kuanza hapo kesho.
Kwenye kesi hiyo, mawakili wa Gachagua wanashikilia kwamba hoja ya kutimuliwa kwa mteja wao imechochewa kisiasa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































