#uncategorized

FAMILIA 32 KIMENDE ZAHAMISHWA KUFUATIA MAPOROMOKO

Familia 32 katika eneo la Matathia kaunti ya Kiambu zimehamishiwa maeneo salama kutokana na mikasa miwili ya maporomoko ya ardhi iliyotokea na kuwafunika watu kadhaa.

Gavana wa kaunti hiyo kimani wamatangi amewataka wakazi kutokaribia maeneo yaliyoathirika, akisema hatua ya kuzihamisha familia hizo inalenga kuepusha majanga zaidi.

Ameyasema haya alipokuwa akitoa chakula cha msaada kwa waathiriwa.

Imetayarishwa na: Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *