KENYA KUADHIMISHA MASHUJAA
Serikali imethibitisha kwamba maadhimisho ya sherehe za Mashujaa zinafanyika hii leo licha ya taifa kuendelea na kipindi cha maombolezo ya Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari, msemaji wa serikali Isaac Mwaura amewataka wakenya kujitokeza kwa wingi kuadhimisha sherehe hizo zitakazoongozwa na Rais William Ruto katika uwanja wa Ithookwe kaunti ya Kitui.
Miongoni mwa wageni mashuhuri walioalikwa ni Waziri mkuu wa Msumbiji Maria Benvinda Levy na Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































