#Local News

LIPA HUSTLER FUND AU ‘USALIMIWE’, OPARANYA

Huenda wakenya ambao wamefeli kulipa mkopo wa Hustler Fund wakajipata pabaya baada ya Waziri wa vyama vya ushirika na biashara ndogo ndogo Wycliffe Oparanya kutangaza msako dhidi yao.

Akizungumza jijini Nairobi, Oparanya amesema wizara yake imeanzisha mchakato wa kubuni mfumo utakaofanikisha kuwanasa wakenya hao, na kupongeza hazina hiyo akisema ililenga kubuni nafasi za ajira.

Wakati uo huo, Oparanya amesema serikali itaanza kuwatuza wakenya ambao wamekuwa wakilipa mkopo huo kwa wakati.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

LIPA HUSTLER FUND AU ‘USALIMIWE’, OPARANYA

WANAFUNZI WALALAMIKIA KATEGORIA TATA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *