FAMILIA ZA MKASA MALAHA ZAJIANDAA KWA MAZISHI
Familia zilizowapoteza jamaa zao kwenye mkasa wa ajali katika eneo la Malaha Junction kwenye barabara kuu ya Webuye kuelekea Kitale zimeanzisha mipango ya mazishi ya wapendwa wao, huku majonzi yakiendelea kutanda katika vijiji hasa Sipala, kilichowapoteza watu 9 usiku huo.
Waathiriwa 6 kati ya jumla ya 15 ni ndugu wa familia moja ya David Kimisu, wengine watatu kwenye Kijiji hicho wakiwa jamaa za familia hiyo ambayo imetaja vifo hivyo kuwa pigo kwao.
Mansura 16 wanaendelea kupokea matibabu hospitalini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































