#Local News

NG-CDF YAELEZWA KUWA MKOMBOZI WA ELIMU VIJIJINI

Wakenya wametakiwa kuunga mkono mswada wa marekebisho ya Katiba unaolenga kuidhinisha rasmi Hazina ya Maendeleo ya Maeneobunge (NG-CDF) kuwa sehemu ya Katiba.

Wakazi wa eneobunge la Malindi, Kaunti ya Kilifi, wameeleza kuwa hazina hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa jamii, hasa kwa kuwasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia maskini kupata elimu.

Aidha, wamesema kuwa fedha za NG-CDF zimechangia pakubwa katika kuboresha miundombinu ya shule mbalimbali, jambo ambalo limeimarisha mazingira ya ujifunzaji na kuongeza ufaulu miongoni mwa wanafunzi.

Imetayarishwa na Janice Marete

NG-CDF YAELEZWA KUWA MKOMBOZI WA ELIMU VIJIJINI

OLUOCH AOMBOLEZA PAUL OTULA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *