WAKENYA WATAKIWA KUCHUKUA PASPOTI JUMAMOSI

Idara ya uhamiaji imewataka wakenya waliotuma maombi ya paspoti jijini Nairobi na walmepokea jumbe za kuwataka kuchukua paspoti hizo kufanya hivyo katika jumba la Nyayo House jijini Nairobi hapo kesho.
Taarifa ya idara hiyo inajiri kufuatia changamoto ambazo zimezingira utoaji wa paspoti kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Kwa sasa, kuna afisi nane pekee za uhamisho kote nchini, hatua inayowalazimu wakenya kusafiri kwa mwendo mrefu kusaka stakabadhi hizo
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































