#Local News

HAKUNA WIZI WA MTIHANI, WIZARA YAKANA

Huku uadilifu wa mtihani wa kitaifa wa kidato cha 4 KCSE ukitiliwa shaka kutokana na visa vya udanganyifu, serikali imesema kwamba mtihani huo uko salama kwamba hakujakuwa na udanganyifu wowote.

Akizungumza kwenye kaunti ya Meru mapema leo, katibu katika wizara ya elimu Dakta Belio Kipsang amesema majaribio ya wizi yamezimwa huku akiongeza kuwa karatasi za mtihani ambazo zimekuwa zikisambazwa mitandaoni ni ghushi.

Aidha Kipsang ametoa hakikisho kwamba masomo ya gredi ya 9 yanayoanza Januari yataendelea bila tashwishwi.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

HAKUNA WIZI WA MTIHANI, WIZARA YAKANA

RUTO AJITETEA DHIDI YA VIONGOZI WA KIDINI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *