#Football #Sports

ENZO MARESCA AMEZEWA MATE NA CHELSEA

Chelsea wanafanya mazungumzo ya kumfanya Enzo Maresca wa Leicester kuwa kocha wao mkuu mpya.

Muitaliano huyo, ambaye hadi mwaka jana alikuwa msaidizi wa Pep Guardiola katika mabingwa wa Uingereza Manchester City, anatarajia  kurejea mara moja kwenye Ligi ya Premia baada ya  Foxes kushuka daraja miezi 12 iliyopita.

Mtindo wake wa soka pia unasemekana kuwavutia wakuu wa Chelsea, huku ikiripotiwa kua  The Blues waliiomba Leicester ruhusa ya kuzungumza moja kwa moja na Maresca, ambaye waliongeza kuwa ndiye chaguo la klabu hiyo ya London.

Chelsea wanawinda meneja mpya baada ya kuachana na Mauricio Pochettino.

Alitumia msimu mmoja tu kuinoa Stamford Bridge, huku Thomas Frank wa Brentford na Kieran McKenna, ambaye aliiongoza Ipswich kupanda daraja la juu nyuma ya Leicester, pia akihusishwa na nafasi hiyo.

Chelsea ilipoteza fainali ya Kombe la Ligi kwa bao 1-0 dhidi ya Liverpool baada ya muda wa ziada na kuwasukuma Manchester City kabla ya kushindwa katika nusu fainali ya Kombe la FA kwa alama sawa.

Imetayarishwana Nelson Andati.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *