VYUO VIKUU KUANDAMANA KUPINGA MFUMO WA UFADHILI WA ELIMU YA JUU

Viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali humu nchini wameendelea kuishinikiza serikali kubadilisha au kufutilia mbali kabisa mfumo wa ufathili wa elimu ya juu la sivyo watalemaza shughuli za masomo katika vyuo vikuu.
Wanafunzi hao wanapendekeza kupunguzwa kwa riba inayotozwa kwenye mikopo ya elimu ya juu kutoka asilim ia 4 hadi asilimia 2.
Iwapo matakwa hayo hayatatekelezwa wanafunzi hao wanasema kuwa watashiriki maandamano septemba tisa mwaka huu.
Imetayarishwa na Janice Marete