#Business

WADAU KATIKA SEKTA YA MADINI WALALAMIKIA KUBAGULIWA

Wadau wa sekta ya madini wamekashifu ubaguzi katika utoaji wa vibali na mfumo wa udhibiti usiofaa ambao unadhoofisha uwekezaji wa mabilioni ya fedha katika sekta ya uchimbaji madini

Licha ya kuondolewa kwa zuio la miaka minne la kusitishwa kwa leseni, Oktoba mwaka jana, wawekezaji katika sekta hiyo wanakabiliwa na changamoto ya kupata vibali vinavyohitajika kutoka kwa wizara hiyo, kutokana na kile walichokitaja kuwa ubaguzi katika utoaji wa vibali.

Chama cha Wachimba Madini nchini (KCM) tangu wakati huo kimetoa wito kwa Rais William Ruto kuingilia kati na kushughulikia “urasimu” katika wizara hiyo, ambayo inawaumiza wachimbaji wakubwa ba wadogo wa madini kote nchini.

Kulingana na chama hicho, ambacho kinawakilisha maslahi ya wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa, wagunduzi, watafiti, wafanyabiashara, wasindikaji, watoa huduma na wataalamu nchini Kenya, utendaji wa sekta hiyo umekuwa ukishuka kutokana na kupungua kwa shughuli za wawekezaji.

Hii inathibitishwa na data ya Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya Kenya (KNBS), inayoonyesha sekta ya madini na uchimbaji mawe ilirekodi upungufu wa asilimia 6.5 mwaka wa 2023 na utendakazi duni mwaka huu, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 9.3 mwaka wa 2022.

Imetayarishwa na Maureen Amwayi

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *