UIGEREZA YAILAZA UHOLANZI 2-1
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amekiri kwamba kikosi chake hakikuwahi kupata mchezaji wa kudhibiti kiungo cha kati kama kinda Kobbie Mainoo kwa muda mrefu sasa.
Mainoo alikuwa mmoja wa wachezaji walioleta tofauti kubwa uwanjani wakati wa pambano la nusu fainali bali ya Uingereza na Uholanzi.
Katika mechi hiyo, Uingereza walitoka nyuma na kuchukua ushindi wa 2-1 dakika za mwisho na kujikatia tikiti ya kuingia kwenye fainali ambayo itachezwa Jumapili dhidi ya Uhispania ambao waliwabandua Ufaransa siku mbili zilizopita.
Alianza kucheza Ligi ya Premia Januari 2023 akiwa na umri wa miaka 17, na akafanikiwa tu msimu wa 2023-24 akiwa na klabu yake.
Mainoo alikua mchezaji mdogo zaidi wa England kucheza nusu fainali ya mashindano makubwa na alionyesha kwa nini Southgate ameweka imani yake kwake.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































