MMELEMAZA AFYA, AYACKO AISUTA HAZINA KUU

Gavana wa Migori Ochillo Ayacko ameikashifu hazina ya kitaifa kwa madai ya kuhujumu utekelezaji wa mpango wa afya kwa wote kutokana na ukosefu wa fedha kwenye serikali za kaunti.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa vituo vya afya kwenye kaunti hiyo, Ayacko amefadhaishwa na uchelewashaji wa mara kwa mara wa utoaji wa mgao wa kaunti na hivyo kulemaza huduma muhimu.
Aidha, amekariri kwamba kaunti zinakabiliwa na madeni na kufanya vigumu kutoa huduma kwa wagonjwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa