#Football #Sports

TUTAUNGA KOCHA MPYA MKONO

Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Hussein Mohammed amethibitisha uungaji mkono wa
serikali kwa shirikisho hilo na michezo.

Siku ya Jumatatu baada ya kuzindua uteuzi unaotarajiwa na unaokisiwa sana wa Benni McCarthy wa
Afrika Kusini, Mohammed alisisitiza dhamira ya serikali ya kuendeleza soka nchini Kenya.

Tangu kuchukua wadhifa huo, utawala wa Mohammed umepokea maoni chanya kutoka kwa wadau
mbalimbali wa soka ambao wanaamini kuwa uongozi mpya utarekebisha mchezo huo nchini Kenya
na kuboresha mtazamo wa FKF miongoni mwa mashabiki.

Hata hivyo, uongozi umerithi deni kubwa la Ksh 383 milioni kutoka kwa watangulizi wake, jambo
ambalo limetatiza maendeleo na kutilia mkazo changamoto za usimamizi mbaya hapo awali.t

Katika kikao chake na wanahabari, Mohammed alitoa wito kwa wadau kuunga mkono utawala wake
ambao tayari umeshika kasi ili kuinua kiwango na ubora wa soka nchini Kenya.

Pia alitoa wito kwa mashirika kusaidia timu za taifa, zikiwemo za wanaume, wanawake na vijana, akisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika mchezo huo.

Imetayarishwa na Nelson Andati

TUTAUNGA KOCHA MPYA MKONO

JEZI MPYA YA SHABANA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *