SERIKALI YATANGAZA IJUMAA KUWA HOLIDEI
Serikali imetangaza kesho tarehe 17 kuwa siku ya likizo kwa taifa ili kuwapa wakenya fursa ya kuomboleza kifo cha Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.
Kupitia notisi, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kumuenzi Odinga.
Sherehe za kitaifa kuhusu mazishi ya kitaifa ya Odinga zitafanyika katika uwanja wa Nyayo hapo kesho.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































