#Business

MAHAKAMA KUPATA MAMLAKA YA KUPINDUA MIKATABA YA KAZI KATIKA MSWADA MPYA 

Huenda mahakama zikapata mamlaka makubwa zaidi ya kuondoa kandarasi zisizo za haki na za upande mmoja iwapo Bunge litapitisha Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mikataba (Marekebisho) ya 2025.

Mswada huo unalenga kuruhusu majaji kubatilisha au kurekebisha makubaliano pale ambapo upande mmoja haufai, na hivyo kuashiria mabadiliko kutoka kwa kanuni ya muda mrefu kwamba mahakama hazipaswi kuingilia mikataba iliyotiwa saini kwa uhuru.

Ikifadhiliwa na Mbunge wa Wajir Mashariki Aden Daudi Mohamed, sheria hiyo inalenga masharti ya kandamizi na yasiyofaa ambayo yanatokana na sheria za kawaida za Kiingereza. Inazuia vifungu ambavyo havijumuishi dhima ya kifo au hasara inayosababishwa na uzembe na inaharamisha majaribio ya kuepuka kuwajibika kwa bidhaa zenye kasoro.

Aidha wasambazaji wa bidhaa mbali mbali pia watawekewa vikwazo vya kuzuia dhima katika kandarasi za watumiaji au kutoa huduma kwa kiasi kikubwa tofauti na ilivyotarajiwa, kuimarisha ulinzi kwa watumiaji na biashara ndogo ndogo.

Imetayarishwa na Maureen Amwayi

MAHAKAMA KUPATA MAMLAKA YA KUPINDUA MIKATABA YA KAZI KATIKA MSWADA MPYA 

MASWALI KUHUSU MAN UNITED

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *