MWANAMUME WA MIAKA 25 AFARIKI JIKONI KWA MAMAYE SIAYA
Polisi katika kaunti ya Siaya wameanzisha uchunguzi kufuatia kifo cha mkazi mmoja huko Ugenya.
George Nyaginde Amenya mwenye umri wa miaka 25 amepatikana amefariki jikoni kwa mamake.
Inaarifiwa kuwa marehemu alivamiwa katika kitongoji cha Nyalenya kilichopo Uyunya.
Kulingana na Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Siaya Cleti Kimaiyo, kisa hicho kiliripotiwa katika kituo cha polisi cha kushika doria cha Aboke.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































