JOHO AWAONYA WANYAKUZI WA MAENEO YA UVUVI

Waziri wa madini na uchumi wa raslimali za majini Hassan Joho, amewaagiza wanyakuzi wa maeneo ya uvuvi katika maeneo mbali mbali nchini kuondoka mara moja.
Akizungumza jijini Mombasa, Joho amesema kwamba tayari awaagiza magavana kutoka kaunti ambako shughuli za uvuvi huendelea kushirikiana na makamishna wa kaunti hizo kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa.
Aidha, Waziri Joho amesema wizara yake imejiandaa kisawasawa kukabili suala la uvuvi haramu katika bahari Hindi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa