MAHAKAMA YASITISHA UTEUZI WA ZABLON MOKUA
Mahakama kuu imesitisha uteuzi wa Zablon Muruka Mokua kama jaji wa mahakama ya Afrika Mashariki kuhusu haki kufuatia kesi iliyowasilishwa na chama cha waansheria nchini LSK wakisema hafuzu kuhudumu katika wadhifa huo.
Jaji wa mahakama hiyo Chacha Mwita, ametoa amri ya kuzuia kuidhinishwa kwa Mokua hadi kesi dhidi yake itakaposikilizwa na kuamuliwa.
Mokua ambaye awali alihudumu kama mwakilishi wa wadi, aliteuliwa na Waziri peninah malonza mwezi Aprili, kuchukua nafasi yake Jaji Charles Nyachae aliyejiuzulu mapema mwaka huu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































