WAKAZI TURKANA KUKOSA HUDUMA ZA MAABARA
Huduma za maabara katika hospitali za umma kwenye kaunti ya Turkana zimesambaratika kufuatia mgomo wa maafisa wa maabara wanaohudumu katika wizara ya afya kwenye kaunti hiyo wanaolalamikia mazingira magumu ya kazi.
Wakiongozwa na mwenyekiti wa muungano wao tawi la Turkana Moses Emoit, maafisa hao wamesema hawatarejea kazini hadi hali itakaporekebishwa, ikiwemo kuongeza idadi ya maafisa wa maabara.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































