#Local News

NAIBU GAVANA KERICHO AIBUA MADAI YA UFUJAJI

Naibu Gavana wa Kaunti ya Kericho, Fred Kirui ameibua madai ya kufujwa kwa zaidi ya shilingi milioni 80 katika serikali ya kaunti hiyo, akitaka uchunguzi kufanywa na kuwawajibisha wahusika.

Kirui ambaye amekuwa na utofauti na Gavana Eric Mutai, amesema pesa hizo zililipwa kwa zaidi ya kampuni 33 za kandarasi na usambazaji bidhaa.

Anadai kuwa malipo hayo yalifanyika kati ya Oktoba mwaka jana na Aprili mwaka huu ila bidhaa hizo hazikuwasilishwa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

NAIBU GAVANA KERICHO AIBUA MADAI YA UFUJAJI

BARAZA LA MAGAVANA LALAMIKIA MADENI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *