#Football #Sports

OMALLA ATAJWA KWA KIKOSI CHA COSAFA

Mfungaji bora wa Ligi Kuu ya FKF 2023/24 Benson Omalla ni miongoni mwa wachezaji ambao wamefuzu katika timu ya mwisho ya Kenya ya U23 inayosafiri kwa  Kombe la COSAFA linalotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 26 hadi Julai 7, 2024, nchini Afrika Kusini.

Mshambulizi huyo wa Gor Mahia mwenye umri wa miaka 22 alifunga mabao 19 na kushinda Kiatu cha Dhahabu katika msimu uliomalizika hivi punde.

Vijana wa U18 Aldrine Kibet, Elly Owande, Ibrahim Wanzala na Amos Wanjala pia wamejumuishwa katika kikosi cha mwisho cha Emerging Stars.

Wachezaji ambao wameachwa nje ya timu ni pamoja na beki wa kulia wa Sofapaka, Baron Ochieng, washambuliaji Moses Shummah wa Kakamega Homeboyz, Samuel Kapen wa City Stars na George Gitau anayechezea Middlesborough ya Uingereza.

Kiungo wa Harambee Stars Anthony ‘Teddy’ Akumu, ambaye amekuwa nje ya uwanja kwa miezi kadhaa, na viungo wa Gor Mahia Alfa Onyango na Shariff Musa pia walishindwa kufurukuta.

Kocha mkuu wa Emerging Stars Ken Odhiambo anasema timu hiyo inajumuisha wachezaji wengi walio na umri wa chini ya miaka 23, ili kuwasaidia kupata uzoefu wa kimataifa na uzoefu katika medani ya kimataifa.

Kenya imepangwa kundi B pamoja na Zambia, Comoro na Zimbabwe.

Kenya itazindua kampeni yake dhidi ya mabingwa mara saba wa Kombe la COSAFA Zambia katika Uwanja wa Nelson Mandela Bay mnamo Alhamisi, Juni 27, 2024, saa 7pm EAT.

Kisha timu itasafiri hadi Wolfson Stadium Jumapili, Juni 30, kumenyana na Comoro saa 1 jioni EAT, kabla ya kucheza mechi ya mwisho ya kundi dhidi ya Zimbabwe Jumanne, Julai 2, 2024 saa 1 jioni.

Imetayarishwa na Nelson Andati

OMALLA ATAJWA KWA KIKOSI CHA COSAFA

CITY THUNDER WANGURUMA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *