KENYA MBIONI KUIMARISHA KILIMO
Katika juhudi za kuimarisha utoshelevu wa chakula, serikali ya Kenya imesema iko tayari kushirikiana na serikali ya Uholanzi ili kupiga jeki sekta ya kilimo nchini.
Katika kikao na wawekezaji Zaidi ya 50 wa Uholanzi waliomtembelea jijini Nairobi, katibu katika wizara ya biashara na viwanda Juma Mukhwana, amesema baadhi ya juhudi hizo ni ujenzi wa vituo vya kilimo katika kila kaunti.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































