#Sports

BAJABER INJE YA CHAN

Maandalizi ya Kenya kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024 yamepata pigo kubwa kufuatia kuondokewa na kiungo mshambuliaji, cheche mbunifu Mohammed Bajaber, ambaye amekamilisha uhamisho wa kiwango cha juu kwenda kwa wababe wa Tanzania, Simba SC.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kenya, kiungo mshambuliaji wa Police FC amesaini mkataba wa miaka miwili na mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simbas SC na anatarajiwa kuungana na wachezaji wenzake wapya mara moja kwa ajili ya ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya nchini Misri.

Kuondolewa kwake kunakuja siku tano tu kabla ya Kenya kuanza kampeni ya CHAN dhidi ya mabingwa mara mbili DR Congo mnamo Agosti 3.

Kujibu tukio la hivi punde zaidi, benchi ya ufundi ilitoa mwito kwa haraka kwa kiungo mshambuliaji Brian Michira Jumapili usiku, kwa matarajio kwamba ataziba pengo la Bajaber.

McCarthy sasa atalazimika kurekebisha mpangilio wake wa kimbinu, huku Bajaber akiwa mchezaji wa tatu muhimu kuondoka katika kambi ya timu ya taifa katika wiki za hivi karibuni.

Washambulizi Emmanuel Osoro na Moses Shummah wote waliondoka kwenye kikosi mapema mwezi huu baada ya kusajiliwa na timu za Ligi Kuu ya Zambia.

Kuondoka KWAKE kumezua wasiwasi juu ya uwiano na utayari wa timu, huku Kenya ikitarajia kuanza vyema katika kundi A lenye timu za Morocco, DR Congo, Angola na Zambia.

Imetayarishwa na Maureen Mukhobe

BAJABER INJE YA CHAN

SHA KUSIMAMIA MATIBABU YA SARATANI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *