100 WAENDA “MTEJA” KWENYE MADARAKA
Zaidi ya wakenya 100 walipoteza simu zao kwenye uwanja wa Raila Odinga mjini Homa Bay wakati wa maadhimisho ya sherehe Madaraka za mwaka huu, nyingi ya simu zikiibwa usiku umati mkubwa ulipokuwa ukiingia uwanjani humo.
Haya ni kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa kaunti ya Homa Bay Lawrence Koilem, akisema idara ya upelelezi DCI imewakamata washukiwa 2 huku simu 12 zikifanikiwa kurejeshwa.
Amewataka waathiriwa wa wizi huo kupiga ripoti kwenye kituo cha polisi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































