WAKAZI WA KAPSABET WAOMBA UPANUZI WA BARABARA
Serikali imetakiwa kuchukua hatuza haraka na kupanua barabara kuu ya Kapsabet kaunti ya Nandi kuelekea Chavakali kaunti ya Vihiga, ili kuzuia visa vya ajali vinavyohusishwa na hali mbovu ya barabara hiyo.
Wakizungumza mjini Kapsabet, wakazi, madereva na wahudumu wa boda boda wamelalamikia madai ya barabara hiyo kutelekezwa na idara husika, wakisema ni nyembamba mbali na kukosa sehemu ya wanaotembea kwa miguu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































