#Local News

KENHA YAZUNGUMZIA MPANGO WA UPANUZI WA BARABARA YA KIAMBU

Kuunganishwa kwa barabara ya Muthaiga –Kiambu– Ndumberi yenye urefu wa kilomita 23.5  kunatazamiwa kupunguza msongamano wa magari kati ya kaunti za Nairobi na Kiambu.

Kulingana na taarifa iliyotolewa hapo jana na KENHA ni  kuwa mradi huo unatarajiwa kuongeza upana wa  barabara hiyo jambo ambalo pia litawakikishia wapita njia usalama wao barabarani.

Mamlaka ya Kitaifa ya Barabara Kuu ya Kenya ( KeNHA ), limesema kuwa barabara hiyo itajumuisha barabara za njia 2 pande zote pamoja na njia za abiria .

Imetayarishwa na Jones Koikai

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *