MBUNGE WA JUJA AKAMATWA NA DCI
Mbunge wa Juja kaunti ya Kiambu George Koimburi anaendelea kuhojiwa katika makao makuu ya idara ya upelelezi DCI baada ya kukamatwa ilia toe maelezo kuhusu matamshi yake kwamba serikali ilitumia shilingi bilioni 13 kwenye kampeni za aliyekuwa mwaniaji wa AUC Raila Odinga.
Kukamatwa kwake kumejiri muda mfupi baada yake kudai kuwa magari mawili aina ya Subaru yalikuwa yameegeshwa nje ya makazi yake katika eneo la Juja.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































