MAUAJI UON: DCI YAZIDISHA UCHUNGUZI
Maafisa wa idara ya upelelezi DCI wameimarisha uchunguzi dhidi ya mshukiwa wa mauaji ya mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi Jane Atila, Nicholas Mutua, baada ya kuibuka kwamba mshukiwa anahusishwa na dhuluma dhidi ya waathiriwa zaidi.
Kulingana na waathiriwa waliojitokeza hapo jana, mshukiwa aliwavamia na kuwatesa katika msitu wa KEFRI eneo la Kikuyu, akiwalazimisha wampe fedha.
Nayo familia ya Atila imesema mwanao aliuawa baada yao kushindwa kumpa mshukiwa shilingi 2,500 alizodai.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































