#Local News

MACHOGU AWAPA HABARI NJEMA WAZAZI, WANAFUNZI

Waziri wa elimu Ezekiel Machogu ametangaza kwamba zoezi la kutuma maombi kwa wanafunzi waliofanya mtihani wa KCSE mwaka jana kupokea mikopo na ufadhili wa elimu ya vyuo vikuu na kiufundi litaanza rasmi hapo kesho kupitia njia ya mtandao.

Katika taarifa, Machogu amesema zoezi hilo lilifaa kuanza Jumamosi iliyopita ila likasongeshwa hadi hapo kesho Jumanne kutokana na agizo la serikali kutangaza siku ya leo kuwa siku kuu.

Aidha, Machogu amewahakikishia wazazi na wanafunzi muda wa kutosha kutuma maombi hayo kabla ya tovuti kufungwa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *